Featured

    Featured Posts

Loading...

RAISI JK AWATEMBELEA WAGONJWA-MOI

Rais Jakaya Kikwete akimsalimu na kumpa pole mtoto Ali Abdul (13) kutoka Rufiji, mkoa wa Pwani, aliyetoka kufanyiwa upasuaji wa kuzibua mishipa ya damu siku za hivi karibuni.Ukaribu huu wa Rais umepongezwa na watu wengi ambapo jana pia aliweza kumtembelea mfungwa, Rajabu Maranda anayetumikia kifungo cha miaka 18 gerezani, pamoja na Mwandishi wa Kituo cha Chanel Ten, Salum Mkambala aliyelazwa hospitalini Muhimbili baadaya kupata ajali ya gari. 
Mbali na kumtembelea Maranda, Rais Kikwete alimjulia hali Mwandishi wa Kituo cha Chanel Ten, Salum Mkambala aliyelazwa hospitalini hapo kutokana na kupata ajali ya gari mapema wiki hii eneo la Vigwaza mkoani Pwani akitoka Dar es Salaam kwenda Morogoro na kuvunjika mguu na mkono wa kulia.


Dar es Salaam. Rais Jakaya Kikwete jana alimtembelea mfungwa, Rajabu Maranda anayetumikia kifungo cha miaka 18 gerezani kwa wizi wa fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), aliyelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili akisumbuliwa na tatizo la mgongo.
Mbali na kumtembelea Maranda, Rais Kikwete alimjulia hali Mwandishi wa Kituo cha Chanel Ten, Salum Mkambala aliyelazwa hospitalini hapo kutokana na kupata ajali ya gari mapema wiki hii eneo la Vigwaza mkoani Pwani akitoka Dar es Salaam kwenda Morogoro na kuvunjika mguu na mkono wa kulia.
Wote wawili wamelazwa katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Upasuaji wa Mishipa ya Fahamu (MOI), wakiendelea na matibabu huku afya zao zikielezwa kuimarika kadri siku zinavyozidi kwenda.
Rais Kikwete aliwasili MOI saa 6.40 mchana na kwenda moja kwa moja wodi D aliyolazwa Mkambala kisha alitoka na kwenda wodi aliyolazwa Maranda.
Rais Kikwete alipofika ulinzi uliimarishwa na hakuruhusiwa mtu yeyote kuingia ndani ya wodi hiyo.
Maranda ambaye ni Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na aliyekuwa Mweka Hazina wa chama hicho Mkoa wa Kigoma alifikishwa MOI, Februari 16 mwaka huu kwa matatizo ya mgongo na kufanyiwa upasuaji. Msemaji wa MOI, Jumaa Almasi alisema hali yake inaendelea kuimarika siku hadi siku.
Maranda na binamu yake Farijala Hussein kwa pamoja walipatikana na makosa sita kati ya saba yaliyokuwa yanakabiliwa ya kujipatia Sh2.2 bilioni za EPA.
Maranda na wenzake pia wanatumikia kifungo cha miaka mitatu jela ambayo itakwenda sanjari na kifungo cha awali cha miaka mitano kutokana na kifungo cha miaka mitatu kwa kila kosa, ambayo ni kula njama, kughushi nyaraka, kutumia hati bandia na kujipatia kiasi hicho cha fedha.
Novemba 2012, Maranda kwa mara ya tatu alihukumiwa kifungo cha miaka miwili jela na kuamriwa kurejesha Sh616.4 milioni.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright SINGIDA KWETU
Back To Top