Featured

    Featured Posts

Loading...

UKICHEKELEA KITAMBI UNAKARIBISHA KISUKARI NA UGONJWA WA MOYO! SOMA HII


Kitambi ni hali ya kiafya ya mtu mnene ambapo mafuta ya ziada mwilini huongezeka eneo la tumbo kwa kiasi kikubwa. Mtu akiwa na kitambi anapata athari kubwa ikiwamo kupungua kwa umri. Katika karne hii, hili ni mojawapo ya tatizo kubwa la kiafya duniani. Hata hivyo, tatizo la kitambi kiafya linarekebishika. Katika mawazo ya kizamani na hata sasa katika baadhi ya nchi mtu akiwa na kitambi anaonekana ni tajiri. Tatizo la unene na vitambi litazidi kuongezeka ikiwa serikali, hususan wananchi wenyewe hawatachukuwa hatua za dharura na mipango madhubuti kulikabili. 
Vitambi hupunguza maisha ya watu wenye hali hiyo ya afya, hivyo kusababisha upotevu wa rasilimali-watu. Ili kuepukana na athari hiyo watu wahakikishe wanabadili namna wanavyoishi. Wengi wana muda mchache sana wa kutayarisha vyakula visivyo na mafuta mengi majumbani mwao, hivyo wanakula nje zaidi, yaani kwenye hoteli na migahawa na matokeo yake ni kuwa na vitambi. Kuna wengi wanatambua athari za tatizo la unene na vitambi, lakini hawafanyi chochote kulirekebisha, hii inatokana na ukweli kwamba idadi kubwa ya watu hawajui maana halisi ya kuwa na afya njema. 
Watu wengi, hasa vijana wamekuzwa kwa kula chipsi, mikate na vyakula vya sukari na si mbogamboga na matunda. Ukweli ni kwamba watu wengi hawafanyi mazoezi ya kutosha kama ilivyokuwa zamani hivyo, watu wenye vitambi wanaongezeka kila sehemu. Nchini Marekani utafiti umefanywa na kugundulika kuwa asilimia 86 ya watu wazima nchini humo watakuwa na vitambi ifikapo mwaka 2030 iwapo hali hii ya kutozingatia masharti ya afya kuhusu unene itaendelea, kufuatana na utafiti wa mwaka 2008 uliofanywa na mtafiti mmoja wa Chuo Kikuu Cha John Hopkins. Ongezeko la tatizo hili la kiafya katika nchi nyingi linatisha. Kwa ujumla, umri wa mtu mnene mwenye kitambi huwa pungufu kwa miaka 8 hadi 10 ukilinganisha na mtu mwenye umbo la kawaida.
 Magonjwa yenye uhusiano na kitambini moyo, aina fulani ya kisukari, magonjwa ambayo huua mamilioni ya watu duniani kote. USHAURI Kila mtu aepuke kula vyakula vyenye mafuta mengi na kutokula chakula kupindukia na ule unaposikia njaa, kutotia mafuta mengi kwenye chakula na kutotumia sukari nyingi. Kila mtu anatakiwa kufanya mazoezi ya kukimbia, kutemba au kuogelea angalau kwa nusu saa kila siku. Watu wanashauriwa kuacha kutumia vyakula vya kopo na hasa vile vyenye gesi nyingi. Wale ambao ni wanene kupita kiasi waonane na daktari kwa ushauri wa kitaalamu.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright SINGIDA KWETU
Back To Top